Watu wengi hutamani sana kupandishwa vyeo baada ya kuchoka sana na nafasi walizokuwa nazo kwa muda mrefu, au pia wengine wanatamani sana kupandishwa vyeo kwasababu ya kuongeza kipato ili kufikia malengo fulani maishani, kilammoja ana sababu binafsi ya kuhitaji kupandishwa cheo. Taarifa za kupandishwa cheo ni za kufurahisha kwa kila mmoja wetu, wako ambao kuilazimisha fursa hii hata kwa kwenda kwa waganga, kuhonga, kujipendekeza, kujitoa miili yao na njia nyingine nyingi ili tu kupata cheo. Mara nyingi tumejiuliza kwanini sipandi cheo, wengine wapya wanakuja hapa wanafanya kazi kidogo mara wanapandishwa cheo, wanabadilishiwa ofisi, wanapata gari la ofisi, nyumba, na marupurupu mengine lakini sio mimi, ukweli ni kwamba sababu kubwa ni sisi wenyewe, vitu vinavyotuangusha na kutufelisha sio vile vilivyo nje yetu bali vile vilivyo ndani yetu, yaani vilivyo ndani ya uwezo wetu. Leo unaweza kuamua kufanya jitihada binafsi za jujua namna ya kuweza kupandishwa cheo. Yamkini wewe ni mmoja wa hawa ninaowazungumzia hapa ili uweze kujikwamua
Jaribu kufuata kanuni hizi rahisi:
1. Jitahidi kujuana na watu.
Unaweza kufikiri kuwa njia pekee ya kubadilisha mazingira uliyonayo ni kukaa na kuwaza sana, hapana, hii siyo kweli, jaribu kujipenyeza kufahamiana na wengine, usijitenge sana, shiriki maisha yako na wale walioko karibu nawe.
Usifikiri kuwa wewe hustahili kujichanganya katika mazungumzo ya kawaida na watu wa ofisini kwako, usifikiri kuongea na bosi wako masuala ya kawaida ni kujipendekeza, kumbuka kwa kuwajua na kujichanganya na wafanyakazi wenzako tunajenga nguvu ya umoja wa kazi, taratibu wote tunakuwa ni timu moja katika utendaji.

2. Usijifanye mkamilifi katika kilakitu.
Pia usibaki umefungiwa katika kiti chako au meza yako ya kazi hata zile nyakati ambazo wengine wanapumzika au kujiburudisha, kama kuna hafla ya ofisi na wenzako wanaenda basi shiriki nao, usifikiri wanapoteza muda, kama mwenzako anatukio fulani la furaha nyumbani basi usiche kushiriki, na kama wewe unatukio kama hilo kwako basi wakaribishe wenzako na usisahau kumualika hata na bosi wako pia. Taratibu unapoanza kumfahamu zaidi bosi wako ni mwelekeo mzuri katika kuelekea mafanikio yako.
Usije ukafikiri kuwa haukuumbiwa kufanya makosa, kufanya kosa kupo katika maisha ya mwanadamu. Kama wewe nimtu unayefanya kazi sana sio  kitu cha kushangaza sana ukikosea kitu. Ikiwa unatokea kufanya kosa, basi usikae ukijilaumu nakujiuliza kwanini umefanya kosa bali jifunze, pata somo katika kukosea kule na uendelee mbele. Kama utaweka akili yako yote katika kujichunguza kila kitu unachokifanya iliusikosee basi hata basi wako anaweza kufikiri kuwa wewe nikati ya wanaojifanya wakamilifu katika kila wafanyalo na kinyume chake cheo kikaenda kwa wenzako na sio wewe. Usisahau kuwa waweza kujikuta unafanya vimakosa vingi zaidi wakati unajitahidi kujiweka mkamilifu katika jambo.
3. Kuwa mwaminifu.
Uaminifu ni kitu kizuri na cha maana sana na kinachowashinda wengi wetu. Wakati wowote unapopata nafaasi ya kuongea na bosi wako, kuwa mkweli katika kila neno litokalo kinywani mwako, liwe dogo au kubwa, liwe kuhusu wewe mwenyewe au kuhusu mtu mwingine, kuwa mkweli hata katika yale yanayoonekana kukuathiri wewe, amua kuwa mkweli bila kujali mazingira. Kuwa mkweli katika yale unayoyatamani na katika maswala mazima ya maendeleo ya kazi yako, sio tu unazungumza kile unachofikiri bosi wako angetamani ukiseme.Staili za kuongea zaweza kutofautiana mtu na mtu lakini ujumbe ubaki kuwa wa kweli.

4. Penda mazingira masafi.
Wakati wowote penda kuyaweka mazingira yako ya kazi safi, hatakama ofisi sio ya kuvutia sana lakini bado unaweza kuvipanga vitu katika meza yako au pale unapofanyia kazi vikawa vema na vyenye mpangilio mzuri. Wengine wamekuwa wakijidanganya kuwa kama wakipoteza muda wao kufanyia usafi eneolao lakazi basi mabosi wao wataona kuwa hawana kazi za kutosha za kufanya, hii ni kinyume kwa maana hali yako ya ndani ya kiutendaji yaweza kuonekana pale tunapotazama mazingira ya wewe unapofanyia kazi.
Maranyingi wengi wetu tumejidanganya kuwa kwa kufanya kazi masaa mengi sana, kutoka usiku makazini na kuwahi kufika mapema sana asubuhi ndio tunaandaa mazingira ya kupanda vyeo, bado kuwaza hivi ni kosa. Ukiendelea hivi kwa muda wanaokuzunguka pamoja na bosi wako wanapata ujumbe kuwa unahangaika sana na majukumu yako yanayoonekana kukushinda na hivyo itakuwia ngumu sana kukabidhi kazi katika wakati muafaka.
5. Fanya kazi katika masaa sahihi.
Kama unadhani unahitaji kufanya majukumu ya zaidi ili upate changamoto za ziada basi inakubidi ukubali kujitolea kutoa msaada katika baadhi ya majukumu ya wengine pale inapobidi. Waweza kuzungumza na bosi wako kuhusu hili pia, jitahidi  kuwa halisi zaidi katika matazamio yako na usiweke malengo yaliyo juu  ya uwezo wako ka unajua hutoweza kuyatimiza.
6. Jitahidi kufanya majukumu ya zaidi.


7. Uliza maswali.
Kukaa kimya tu huku umeinamisha kichwa chini pasipo kusema kitu hakutakusaidia chochote katika kupanda cheo, Usihofu kuuliza swali lolote na kama unakitu au wazo juu ya jinsi gani halifulani inaweza kuboreshwa basi iseme kwa wahusika. Yawezekana ukajiona kama unayepitiliza mipaka yako ya kazi, na yamkini wengine wasikuelewe, lakini usihofu maana taratibu itawaonyesha kuwa unaipenda kazi na uko tayari katika kuboresha biashara au mafanikio ya ofisi kwa ujumla.
8. Fanya utafiti.
Kama unakiu ya kupanda ngazi katika masuala ya kikazi na ajira basi lazima ufanye tafiti, kama kuna kazi maalumu unataka kuiomba hakikisha unajua kilakitu kuhusu kazi hiyo na uweze kuelezea jinsi gani ujuzi wako unaendana na ule unaohitajika katika kazi husika.
9. Jifunze kutengeneza nafasi mpya
Kama unafikiri kuna njia rahisi zaidi au za mafanikio zaidi katika utendaji wako wa kazi au kama unaona umuhimu wa kuwepo kwa nafasi nyingine ya kazi ni bora uzungumze na bosi wako. Kwa sababu wewe ndiyo uliyeona umuhimu wa nafasi hiyo na kulitolea wazo, kuna uwezekano mkubwa kwamba wewe ndiyo utakayeonekana kufaa kuchukua nafasi hiyo, hii inamaanisha kwamba utakuwa tayari kubeba majukumu mapya.

10. Ongeza ujuzi wako.
Kama unaona kunaumuhimu wa kuongezea kidogo ujuzi ulionao basi tafuta kozi zinazoendana na kile unachotaka kukifanya, jitahidi kuhudhuria semina, warsha na makongamano mbalimbali ya mlengo wa kazi yako, penda kujua zaidi ya vile wenzako wanavyovijua. Waweza kuwauliza waajiri wako kama kuna fungu kwa ajili ya kujiendeleza ili ulifaidi, onyesha kuwa unakiu ya kujiongezea ujuzi kwa manufaa ya kampuni au ofisi, hii itawafurahisha wakuu wako na kupanua wigo wa kukufikiria kwa majukumu makubwa zaidi.

Onyesha mafanikio yako kwaundani iwezekanavyo lakini pasipo kujikweza au kujisifia, mfano; kama umefanikiwa kuvuka malengo ya mauzo yako kwa kipindi fulani, basi acha mabosi wako walijue hilo.Mara uchukuapo jukumu fulani ilikulifanya basi jitahidi kuonyesha kuwa unalifurahia na wala haulijutii, fanya kila ulilosema kuwa utalifanya, na kwa hivyo utaonyesha heshima kubwa na kujionyesha mtu unayeweza kutegemewa. Ni muhimu sana kuwa na tabia hizi kwa maendeleo binafsi.

Na: Chris Mauki
University of Pretoria
South Africa
chriss@udsm.ac.tz

Categories:

Leave a Reply