http://lh4.ggpht.com/-SvfDvGheaNQ/UgePsAn4eAI/AAAAAAAAA4k/aB71DpBFM9g/s1600/utajiri%25255B2%25255D.jpg




IMEANDIKWA NA MAKIRITA AMANI WA AMKA MTANZANIA 
 Wengi tunajua matajiri wakubwa wa Tanzania, wa Afrika na hata wa dunia kwa ujumla. Na baadhi yetu tunajua thamani ya utajiri wanaomiliki matajiri hawa, japo yule wa kwanza. Huenda umeshawahi kuingia kwenye ubisha na wenzako kuhusu nani tajiri namba moja ama kiwango cha utajiri matajiri wakubwa wanachomiliki.
  Ni vizuri sana kujua takwimu hizi za watu matajiri, ila je umewahi kuziandika takwimu za utajiri wako? Ama unafikiri huna utajiri unaoweza kuuandikia takwimu? Ama unafikiri kwakuwa huna fedha walizonazo matajiri wakubwa basi wewe huna utajiri wowote unaomiliki?
utajiri
  Kama unafikiri wewe sio tajiri basi unakosea, kama unaweza kusoma hapa basi wewe unamiliki utajiri mkubwa sana.
  Hebu kaa chini na utathimini thamani ya vitu hivi ambavyo umepewa bure kabisa.
  Maisha, unaweza kusoma hapa kwa sababu unaishi, na una afya njema. Je akitokea mtu mwenye fedha nyingi akakuambia umuuzie moyo wako utamwambia akupe shilingi ngapi?(soma; thamani ya uhai wako). Maisha yako na afya yako ni utajiri mkubwa sana kwako.
  Viungo vya mwili ulivyonavyo, akili timamu, macho, masikio, mikono na miguu. Ni gharama kiasi gani unaweza kumtoza mtu atakaetaka kununua baadhi ya viungo hivyo kutoka kwako? Kama una viungo hivyo na vinafanya kazi vizuri basi wewe ni tajiri mkubwa sana. Hata kama kuna vyote ila kuwa tu una akili timamu ni utajiri tosha. Kuna watu wengi ambao hawana baadhi ya viungo kama mikono, miguu, ama macho ila wamefanya mambo makubwa sana. (Soma; kama unadhani wewe una bahati mbaya na nini hasa ulichokosa)
usikate tamaausikate tamaa3
  Jua thamani ya utajiri unaomiliki ili uweze kuubadili kuwa utajiri wa kifedha. Tumia ulichonacho na vinavyokuzunguka ili kufikia mafanikio unayotaka. Umasikini ni hali ya fikra na wala sio kukosa umiliki wa vitu.

Categories:

Leave a Reply