Mara baada ya kupata Tip#3 kwamba kila kijana anapaswa kuelewa umuhimu wa Kujithamini (Self-esteem) na Kujiamini (Confidence) na kuwa mambo haya mawili yanaweza kumjenga na kumbomoa mtu. Tulielezea baadhi ya mambo yanayoendelea kichwani mwa mtu asiyejiamini wala kujithamini (negative self-talk) huchangia katika kumrudisha mtu nyuma katika maendeleo yake binafsi.

Unataka kujua jinsi ya kujisikia vibaya na nafsi yako? Tunakudokezea kiduchu mambo yatakayo kufanya ujisikie vibaya - tena vibaya kinoma kuhusu wewe na nafsi yako.

i) Jilinganishe wewe na kila mtu au kila kitu kilichokuzunguka. Chagua vitu walivyonavyo ambavyo huna. Fikiria jinsi walivyo na bahati na wewe ulivyo na mkosi

ii) Ukipata fursa yeyote ya kujiangusha, wewe jiponde tu. Epuka kusema au kuamini kuwa wewe ni mtu wa pekee na huna kasoro yeyote ile

iii) Kataa unaposifiwa. Waambie watu kuwa “ni kitu kidogo tu hicho, usijali…” au wewe sio mtu wanaostahili kumpa sifa au pongezi. Usimshukuru mtu yeyote anapokusifia, jifanye kama hujasikia.

iv) Kila mara jiambie “mimi ni balaa tupu”, “mimi mjinga”, “sina mvuto”, “sipendwi” au “sifai”.

v) Jichanganye au jihusishe na vitu ambavyo vitakuangusha, kudhalilisha na kukuvunjia heshima. Hii itasaidia hayo yaliyotajwa hapo juu kuzama ndani yako zaidi.

vi) Kaa kila mara na orodha ya mambo yaliyosababisha uanguke, ufeli, kukuaibisha, mambo uliyokosea na uziweke kwenye kumbukumbu zako kwenye diary yako, chumbani umezibandika au sehemu yeyote unayotaka wewe.

vii) Jitenge, kaa kivyakovyako na usizoeane na watu wala usitake watu wakujue jue. Acha kumsifia mtu, kusaidia watu wala kuchangia katika shughuli yeyote ile.

viii) Epuka kitu chochote kinachokuburudisha na unachopenda kufanya.

ix) Ishi maisha yako kwa kuwaridhisha watu wengine. Fanya maamuzi yako yote kutokana na vitu watakavyo idhinisha na watakacho kifurahia

x) Usifanye kitu chochote kigeni kwenye maisha yako. Kaa nyuma na usubiri miujiza au kitu kitokee na kiweze kuyabadilisha maisha yako.

Kuna wakati mwingine, tena bila hata kujitambua wenyewe, tunajikuta tunafanya maamuzi ya kujiumiza tu. Hali halisi ni kuwa ungependa kukaribisha hisia za kujiamini na kujithamini katika maisha yako.

Kuna njia nyingi sana za wewe kukaribisha hali ya kujithamini ndani ya maisha yako. Badili kwanza fikra na mtazamo wako. Jipende wewe binafsi! Acha kujiadhibu na kujipa wakati mgumu na anza kwa kujipongeza mwenyewe. Matatizo, dhiki na shida za dunia zipo tangia enzi za manabii na zitaendelea kuwepo siku nyingi baada ya wewe kuiaga hii dunia. "This is your time, we only live once, live and embrace life". Wewe ni mtu ‘unique’ kwenye hii dunia. Hakuna mwingine kama wewe kati ya watu billion 7 duniani. Nenda China, Nigeria, Rwanda au India ukatafute mtu mwingine aliye kama wewe kabisa! Hakuna kama wewe.... uko peke yako - a ‘unique’ being. Zaidi ya mama aliyekuzaa, nobody atakupa ‘first class’ love zaidi yako mwenyewe kwanza. Jipende mwenyewe kwanza, ili wengine wakupende vilevile. Ukianza kujilinganisha na wengine au mwingine, lazima utajikuta unayo mapungufu kimaumbile, kimapato, na kwenye maisha vile vile.

Hayo mambo 10 tuliyo orodhesha hapo, uyatumie kuyabadilisha yawe katika "positive self-talk" na kama kichwa chako kina mitazamo hiyo 10, uzifute moja moja kila siku kuanzia sasa, ili baada ya siku 10, hata moja tena zimetoweka kichwani mwako. Achana na feelings za kukupa ‘low self-esteem', hazitokusaidia chochote katika maisha yako. Usiache ikatambaa na kukuganda na kukuharibia maisha yako. Pigana kuanzia sasa na ubadilike uwe na mtazamo chanya. Kumbuka, hakuna SIRI ya utajiri wala mafanikio, uliza kila mtu mwenye mafanikio ya hali ya juu. Ataanza kukuambia, fikra, fikra, fikra... fikra zako ndizo zitakazo kujenga au kukubomoa.

Tembelea ukurasa wetu kesho tukijaaliwa tutazungumzia mbinu zitakazokusaidia katika kujijengea tabia za kujiamini na ujifunze jinsi ya kuzifanya ziwe za kudumu katika maisha yako. Tunakutakia siku njema!

kwa hisani ya shear illusions

Categories:

Leave a Reply