UFUPISHO.

Samuel na Sadiki wametoka katika familia zilizokuwa za dini. Samuel alikuwa mtoto wa mchungaji Kipelele wa kanisa la Praise and Worship lililokuwa mwenge jijini dar es Salaam huku Sadiki akiwa mtoto wa Imamu wa msikiti wa kichangani uliokuwa magomeni jijini Dar es Salaam. Wote wanasoma katika shule ya Uhuru mkoani Kilimanjaro. Kutokana na kupenda sana dini, muda wote wanaonekana kuwa watakatifu huku walimu wakiwataka wanafunzi wote shuleni hapo waige maisha yao.
Mambo yanaonekana kubadilika, uwepo wa msichana Catherine Mushi na Mariamu Saidi unaonekana kuanza kubadilisha kila kitu. Wote wawili wanajikuta wakiangukia katika ulimwengu wa mapenzi, wanaziacha dini zao, wanagoma kwenda msikitini na kanisani. Mapenzi hayo yaliyowafanya kuziacha dini zao ndio mapenzi ambayo yaliwafanya wawili hawa kuingia katika mtafaruku mkubwa, mtafaruku ambao unaibua chuki kubwa mioyoni mwao huku wakiwa wamejiingiza katika kitu ambacho kiliwapa utajiri mkubwa ambao kwa muonekano tu, haukuwa utajiri wa halali kabisa.
MAPENZI. Yakawafanya kuchukiana, mapenzi yakaonekana kusababisha kifo maishani mwao, ila hayo hayo mapenzi, yaliwafanya kumsahau MUNGU wao.

Unajua nini kilitokea katika maisha ya watu hawa?
Pata nakala yako.
Kitabu kitatolewa siku ya Ijumaa. Kwa wakazi wa dar es salaam watafikishiwa walipo na kwa wakazi wa mikoani, watatumiwa huko huko kupitia kwa mawakala wetu. Kitabu kimoja kitapatikana kwa sh 7000/= tu. Kama unataka kuweka oda na kupata maelezo mengine unawaza kupiga simu hii 0718 069 269.

Categories:

Leave a Reply