Biashara nyingi sana huwa zinakufa baada ya wamiliki wake kufariki, But kwa uchunguzi wangu ni zile zinazo milikiwa single, soleproprietorship ndo huwa zinakufa sana na si hapa Tanzania tu, make ukiwa wewe ndo mmiliki pekee ukifa maana yake Biashara lazima fe make sheria haziruhusu mwingine kuimiliki papo kwa hapo

SABABU ZA KWA NINI ZINAKUFA

1. Wamiliki wengi kuto kuweka msingi mzuri wa Biashara zao base kiasi kwamba hata akifa au akiugua muda mrefu ziendelee kuwepo,

2. Kwa wamiliki mmoja mmoja kuto kuandaa warithi mapema sana, hapa ndo kuna shida kubwa sana,
- MMILIKI KUWA MSIMAMIZI WA KILA KITU
- KUTUMIA WAKE ZAKE/WATOTO/NDUGU NA JAMAA KUSIMAMIA BILA KUWAJENGEA UWEZO
- kUSHINDWA KUANDAA SUCCESSION PLAN YA NANI ATAKUWA KIONGOZI WA HII BIASHARA PINDI NIKIFARIKI
- Kuachia kikao cha mirathi kuamua nani wa kusimamia biashara ya marehemu bila kuangalia uwezo wa mteuliwa nayo factor kubwa sana
- Mmiliki kuto kuwaendeleza watoto wake/mke/ndugu katika elimu ya biashara ili kuwajengea uwezo wa kibiashara wa kusimamia baishara na hivyo kuaha wasimamie kimazoea tu
- Kutumia uchawi katika biashara inyo pelekea ukifa na nguvu za giza za biashara yako zinafikia tamati

SULUHISHO NI NINI?

1. Tujitahidi kuwa na makampuni na si kuendesha individual hii inaweza kuwa suluhisho


2. Kuwajengea uwezo wasimamizi wa biashara yako tangia mwanzo na kuwaelimisha mambo mbalimbali yahusuyo biashara yako

3. Kuandaa succession plan mapema sana ya nani atasimamia hii biashara pindi nikifa, na huyo aliyoko kwenye plan aandaliwe mapema kielimu na si mtu aliendaliwa aachwe akasomee kosi zingine tofauti na za biashara, hapa mmiliki ahakikishe mtoto wake atakaye mrithi anakua na mwelekeo wa masomo ya biashara sana na si mtoto anatazamiwa kurithi biashara za baba huku yeye achukua Degree ya KISWAHILI AU KITU KINGINE KISICHO ENDANA NA BIASHARA

4. Kuwapa wasimamizi wako mazoezi ya vitendo means wawe wasimamizi kuanzia ukiwa bado hai na uwe mshauri wao tu, MFANO WAHINDI, VITOTO VYA WAHINDI VINAJUA BIASHARA VIKIWA BADO VIDOGO SANA TENA PRACTICALLY SIO THORETICALY
Categories:

Categories:

Leave a Reply