UTAKUWA
na tofauti gani katika maisha yako endapo utakuwa mtu wa kujiamini? Ni
nini zaidi utakachokipata? Hilo ni swali ambalo sote tunaweza
kujiuliza.
Ni ukweli usiopingika, kwamba hali ya kujiamini
inasitawisha maisha yako. Hivyo unapokuwa na afya nzuri inakufanya
ufikie malengo yako kwa urahisi zaidi.
Unapojiamini katika maisha
yako na shughuli zako za kila siku, utaweza kuwasaidia na wengine ambao
unawasiliana nao katika maeneo mbalimbali iwe ni nyumbani au kazini.
Vile vile endapo unakutana na mambo ya kustaajabisha, ya kushtusha au ya
mshangao huna haja ya kuogopa, kwa kuwa tayari umeshajijengea hali ya
kujiamini, utaikabili hali hiyo kwa urahisi.
Ni vizuri kujijengea
hali ya kujiamini katika maisha yako kwani watu wote walio na hali hiyo
wamekuwa na viwango vya tofauti ambavyo kila moja anavifurahia. Kumbuka
kuwa hali ya kujiamini na kuwa jasiri, ni muhimu sana katika kila
hatua ya maisha yetu, hivyo watu wengi wanajitahidi kuitafuta.
Kwa
mtazamo mwingine watu waliokosa hali ya kujiamini inakuwa ni vigumu
kwao kupata mafanikio. Kwa upande mwingine, unaweza kushawishika na mtu
anayezungumza kwa ufasaha, anayejibu maswali yake kwa kujiamini na
anayekuwa tayari kukubali kwamba jambo fulani halifahamu.
Mtu huyo ni
rahisi kujifunza jambo jipya ambalo litamwongezea mafanikio zaidi
katika maisha yake kwa kuwa yuko tayari. Watu wanaojiamini huambukiza
hali hiyo kwa wengine. Hadhira anayokutana nayo, wanachama wenzake, bosi
wake, wateja wake na rafiki zake.
Kupata ujasiri wa wengine ni njia
mojawapo ambayo mtu anayejiamini huitafuta kwa ajili ya kupata
mafanikio zaidi. Habari njema ni kwamba hali hiyo unaweza kujifunza na
kuijenga katika maisha yako.
Na endapo unafanya kazi kwa kujiamini
au kuwajengea ujasiri watu wanaokuzunguka, unakuwa umefanya jambo jema.
Mambo mengine yote yanakuwa sawa kutokana na kujiamini kwako, na
yeyote anayejiamini huwa na mafanikio katika maisha yake tofauti na
yule mtu ambaye hajiamini. Kiwango chako cha kujiamini kinaweza
kuonekana katika njia nyingi. Mfano kutokana na tabia yako, lugha yako,
jinsi unavyoongea, kile unachozungumza na mambo mengine mbalimbali.
Unawezaje kujijengea hali ya kujiamini?
Ni kwa kufanya kazi ya kutoa
ushauri katika mazingira ya kushughulika na watu wa aina mbalimbali,
wenye tabia mbalimbali waliovunjika moyo na wanaohitaji msaada zaidi wa
kukabiliana na ugumu wa maisha. Unapofanya kazi hiyo ya kutoa ushauri
unatakiwa kujua njia sahihi ya kukabiliana na mtu mwenye msongo wa
mawazo na kujua ni jinsi gani utaanza mazungumzo naye kutokana na hali
aliyokuwa nayo.
“Wakati nilipokuwa naanza kuangalia jinsi ya kuwa na
hali yangu mwenyewe ya kujiamini, nilijaribu kuangalia maeneo
mbalimbali yatakayonifanya nijijengee uwezo wa kujiamini. Japo kwa mara
ya kwanza ilikuwa ni vigumu, lakini ilichukua muda mrefu na niliweza
kufanikiwa,” alisema John Robert.
Jambo jingine ambalo linaweza
kukusaidia ni kupunguza kumbukumbu za maumivu yatokanayo na mambo
yaliyopita katika maisha yako. Hivyo, kama unataka kusonga mbele
usikumbuke mambo yaliyopita ambayo yatakurudisha nyuma. Japo ni vizuri
kujifunza kutokana na mambo yaliyopita lakini huhitaji kuendelea kuwa
na kumbukumbu zinazoumiza.
Ni vyema kama hautafikiria yaliyopita.
Hivyo, unaweza ukawa umejifunza wewe mwenyewe mbinu za kujiamini,
unapoamua kubadilika na kuwa jasiri, ni kwamba pale unapoanza,
utaendelea kukua na kukua.
Unaweza kuendelea kuhisi kwamba pengine
unaweza kujiamini zaidi, maisha yanaweza kuwa mazuri kutokana na hali
hiyo. Hivyo, mwishoni unafikia ndoto zako kama vile kupata kazi kubwa,
kuwa na mahusiano mazuri, kununua nyumba na mambo mengineyo. Unajisikia
vizuri wewe mwenyewe na kuwa na furaha kutokana na kile unachokipata.
Zipo njia mbalimbali zinazoweza kukufanya ujiamini. Baadhi ya njia hizo
zinafanikiwa na nyingine zinashindwa kutokana na mtu mwenyewe.
Wakati
mwingine unaweza kujisikia kuwa unahitaji msaada, mtu wa kuongea naye,
au kutafuta njia rahisi na kutoa ushauri bila kulipa pesa nyingi. Ni
njia ya muda mrefu kuweza kuwa na hali hiyo ya kujiamini lakini inaweza
kuwa ni safari nzuri kwa sababu inabadilisha maisha yako. Pia
inashangaza kwa sababu unaweza kunufaika zaidi katika kila hatua
unavyoongea.
Je, uko tayari kujijengea hali ya kujiamini? Kwanza inakupasa kufanya shughuli mbalimbali ambazo zitakujengea uwezo huo.
“Fanya
shughuli za kukujengea ujasiri kila siku na kuwa na mawazo
yanayoipanua akili yako,” anasema Mike Bonny. Pia unaweza kujiuliza ni
kwa kiasi gani una ujasiri? Hali hiyo inaweza kuwepo kutokana na afya
katika akili yako. Kwa mfano, kama unajisikia uchovu muda wote, itakuwa
ngumu kuwa jasiri.
Ujasiri katika kufikiri ni jinsi gani mawazo
yako yanaweza kuyabadilisha maisha yako. Unapokuwa jasiri katika
kufikiri ni sababu ya kuyabadili mawazo tunayoyawaza. Vilevile, ujasiri
katika mahusiano mara nyingine unaweza kuona ni kitu cha kukupa
changamoto.
Sasa basi, unaweza ukaangalia ulinganisho wa tabia ya
kujiamini na ile ya kutojiamini. Ni hatua gani unazoweza kuzichukua
kwako binafsi na kwa watu wanaokuzunguka? Unapokuwa mtu wa kujiamini
unafanya kile unachofikiri ni sawa, ingawa wengine watakukosoa.
Pia
utakuwa tayari kwa lolote ili uweze kupata vitu vizuri. Vile vile
unakuwa ni mtu wa kukubali makosa yako na kujifunza. Mtu asiyejiamini
anakuwa ameegemea upande wa wengine wanavyofikiri. Unabakia kukaa
sehemu moja ukiogopa kushindwa na kukwepa kubahatisha au kuthubutu
kufanya jambo fulani. Anakuwa mgumu kukubali kosa.
Kama ulivyoona
katika mifano hiyo hapo, hali ya kutojiamini inakuletea uharibifu, bali
inakujenga. Jifunze kujiamini, kuwa jasiri katika kila jambo
unalolifanya, usitetereke utafanikiwa.
Categories: