swala la Vijana wa vyuo vikuu kujiajiri lina Historia ndefu sana na ni
mchanganyiko wa factor nyingi sana ambazo ukijumlisha pamoja unakuja
kupata hili tatizo la graduate kushindwa kujiajiri na kuishia kusubiria
ajira za serikali au sekita bianfisi,
1. MFUMO WA UCHUMI WA NCHI YETU, UJAMAA NA KUJITEGEMEA
Huu mfumo ungali vichwani mwa watanzania wengi sana na kibaya zaidi
umekuwa ukirithiswa kwa vijina ambao wamezaliwa baada ya UJAMAA KUWA
UMEANGUKA MIAKA YA 90,
Ujamaa unalemaza sana na Nchi kama Urusi kilicho isaidia kumove
fasta kutoka Uchumi wa kijamaa kwenda uchumi wa huru ni kwa sababu
ilikuwa imeisha jiimarisha kwa viwanda na makampuni makubwa sana na
Ukiangalia uchumi wa URUSI unashukiliwa na Warusi wenyewe
walibinasifisha makampuni yao kwa wao wenyewe,
Ingawa hata urusi Entrpremership culture si kubwa kama ilivyo INDIA na nchi zingine
China kilicho wasaidia ni Kuwa na mifumo miwili kwa wakati mmoja Socialism na Market economy,
Watanzania bado tuko katika huu mfumo wa kijamaa na ndo maana bado
tunaamini Serikali ndo inatakiwa kuwatafutia masoko wafanya biashara,
iwaanzishie biashara, iwaambie waanzishe biashara na kazalika, so watoto
wanakuwa wanaaminishwa kwamba serikali ndo inatakiwa kufanya mambo
mengi sana na wao ni kusoma na kuajiriwa tu.
Nchi kama kenya wao kutokana na kuanza na mfumo wa ubepari tangia wapate
uhuru wao wako juu sana kwa vijana wao kupenda kujijiri kuliko TZ
2. UBINASIFISHAJI MBAYA WA MASHIRIKA YA UMA HASA VIWANDA ULIDESCOURAGE ENTREPRERSHIP CULTURE
Vijana wengi hawana pa kujifunza ujasiriamali kwa sababu Viwanda
vyote walipewa wahindi na hii indescourage sana entreprenership culture
sema tu hatujajua, Tungefanya kama URUSI ingesaidia sana kuhamasisha
vijana waingie katika Ujasirimali, kwa sasa tunajifunz kwa MENGI PEKEE
NA WENGINE WACHACHE, na nivigumu kujifunza kwa makaburu na wahindi.
3. MALEZI YA WAZAZI WETU
Hili ndo tatizo namba moja linalo fanya Vijana wasijiingize kwenye
Biashara/ujasirimali, waswahili wanasema samaki mkunje angali mbichi na
ukiangalia kweli nchi kama India na kwingineko Vijana wanaanza
ujasirimali wakiwa na umuri wa miaka 20 mpaka 38 na huu ndo muda wa mtu
kuingia ktika ujasirimali,
Tangia tukiwa watoto tunasisitizwa tusome sana tuje kuwa MAMENEJA,
WAHASIBU WA MAKAMPUNI, TUFANYE KAZI BENKI, TUWE WAKURUGENZI, TUWE
MARUBANI, na hii ni sumu mbaya sana ambayi kwa kweli inafanya watoto
wakuwe wakiamni wao wanatikiwa kufanya kazi na si kujiajiri,
4. SUCCESSFUL IS GENETIC
Ili kijana aje kuwa mjasirimali mzuri inategemeana sana na ndugu
zake, marafiki zake na majirani zake, kama hawa watu wote nilio wataja
ni Wafanya kazi mtoto atasoma aili aje kuwa kama wao,
Ingawa kuna wachache ambao wanakuwa wajasirimali wazuri pamoja na kwamba
ndugu zao, marafiki, majirani na wafanya kazi, ila kwa kiasi kikubwa
sana hili linachangia sana
5. MIFUMO MI BOVU YA ELIMU YETU
- Tunakaririshwa sana, tunasoma theory sana badala ya Vitndo, kuna
vyuo vinatoa elimu ya ujasirimali, MZUMBE WANATOA DEGREE NA MASTER, UD
WANATOA, UDOM WANATO, ila ukifuatilia wote walio maliza hapo wameajiriwa
na kuna ambao wako mitaani wanatafuta kazi pamoja na kwamba wanaelimu
ya Ujasirimali
6. KUKOSEKANA KWA VIVUTIO,
Ni kweli hakuna vivutio vingi vya kuhamasisha Vijana wengi wajiajiri
wamalizapo masomo na badala yake kuna vitu kama mamilioni ya JK yaliyo
tolewa kisiasa bila kujali kama wanaohitajo wana nia ya kufanya biashara
au la,
Nchi nyingi hasa za ASIA zina vivutio kwa ajiri ya Graduate wao kama
vile , ila huku naona vivutio vya kuwafanya watu wasome SCIENCE lakini
hakuna mikakati ya kuwafanya graduate wajiajiri wamalizapo masomo,
SIJAWAHI SIKIA MZAZI AKIMSISTIZA MTOTO WAKE KWAMBA ASOME AJE KUWA MFANYA BIASHARA MKUBWA KAMA WAKINA MENGI.
Categories: