ELIMIKA NA CHRIS MAUKI............JINSI YA KUMGUNDUA MPENZI MPENDA PESA ZAKO (Knowing a gold digger)
Wengi
wetu tumeingia katika mapenzi na wapenzi wenye tabia tofauti na baadhi
wameshindwa kufahamu kama katika mapenzi hayo wanapata hasara au
wananufaika. Sio kwamba katika mapenzi ni sehemu ya kuingia ukitazamia
faida na manufaa tu, najua ziko nyakati za kujitoa kwaajili ya umpendaye
lakini kwa wastani katika nyakati zote hizi wapenzi wote wawe na furaha
mioyoni na hali ya kujisikia kutoshelezana katika maeneo yote ya maisha
yao ya kilasiku na sio mmoja kujihisi kudhulumiwa, kutotendewa haki au
kuegemewa zaidi kimahitaji.Nimekutana
na lawama na malalamiko mengi sana kati ya wapenzi na hata maranyingine
waliojikuta wameshaingia kwenye ndoa na nimeona nivema nitafute jinsi
ya kuwasaidia wenye tatizo hili au kuku wezesha na wewe kumsaidia na
mwingine.Wako
wapenzi wanawake au wanaume ambao tabia yao nikutafuta namna ya
kuzichimba pesa za mpenzi wake kwa namna yoyote ile. Mara nyingi wanaume
wamekuwa wakiwalalamikia wanawake kuwa ndiyo wanaojifanya wanapenda
kumbe wanachokitaka ni pesa au unafuu wa maisha kiuchumi kutoka kwa
wapenzi wao wakiume. Lakini sikuhizi mambo yamekuwa na uwiano sawa, wako
vijana wa kiume pia ambao kazi yao ni kuwalemea wapenzi wao kila siku
kwa mahitaji yasiyoisha. Leo watasema wanashida hii, kesho shida
nyingine itaibuka, na keshokutwa atakuja na jipya pia. Hali hii
huyafanya mapenzi yakawa butu sana hatakama anayeelemewa hajaweza kusema
kwa uwazi maumivu anayo yapata.
Huyu
mpenzi wakike au wakiume mwenye tabia hizi huwa ndani ya moyo wake
anajijua kabisa kuwa hana mapenzi ya dhati na shida yake ni kuyapunguza
matatizo aliyo nayo, na maranyingine sio kwamba ana matatizo sana ila
baada ya kuona mwanya wa kupata anachohitaji wakati wowote basi
atatafuta hitaji lolote na kulipa umuhimu ili kukuonyesha uharaka wa
kumsaidia. Kamwe haogopi wala kuhofia yeye tu kuonekana ndio mwenye
shida kila siku na wala sio mpenzi mwingine, jiulize, iweje shida ziwe
kwako kila siku tu?Wala
huitaji kuwa tajiri sana ili wapenzi wa aina hii wakuvae, kama
unampenzi wako wa kawaida tu an labda umeshawahi kujihisi kwamba mpenzi
wako anaonyesha dalili za kuipenda hela yako zaidi, basi wewe tayari
unanafasi kubwa ya kuwa mhanga wa wapenzi wa aina hii. Inabidi ujichunge
na kuwa macho sana kwasababu wanapokupata huhakikisha wewe ndio unakuwa
jawabu la maswali yao yote yanayohusu uchumi wao binafsi na
maranyingine hata uchumi wa ndugu zake.
Iko
tofauti kubwa kati ya mpenzi mpenda pesa zako na yule mpenzi ambaye
unamsaidia na anauthamini msaada unaompa na kwamba hakufanya kusudi
kulionyesha hitaji lake kwako ili umsaidie. Mpenzi mpenda pesa yako
huhitaji chochote kutoka kwako na hata baada ya kukipata hauthamini
msaada huo, maranyingine anaweza hata kukudhihaki kama yamkini umempa
msaada chini ya kiwango alichotarajia kukipata kutoka kwako. Sio hivyo
tu, mpenzi mpenda pesa zako anaweza kukuacha kimapenzi pale anapoona
uwezowako wakumsaidia unapungua au kunamazingira ya uwezo huo kupungua
huko mbeleni, mfano; anafahamu umeachishwa kazi, au umesimamishwa kazi,
au umepata hasara kubwa katika biashara yako, au unapitia kipindi
chochote kigumu kimaisha basi yeye badala ya kuumia au kusikitika na
wewe atatafuta namna ya kukukwepa na kukuacha iliyeye akatafute mfadhili
mwingine. Wapenzi wa jinsi hii kamwe hawapendi kusikia eti huna hela,
wao hufurahia uharaka wa wewe kutatua matatizo yao tu.Ukitaka
kumfahamu mpenzi wako yuko mkondo upi basi jaribu kumuuliza maswali
kama vile; Ni zawadi gani ya maana sana amewahi kuipokea? Au ni kitu
gani kikubwa ulichowahi kukiachilia kwa ajili ya mtu au rafiki? Majibu
ya mpenzi mpenda pesa zako yataonyesha vitu vya garama sana na pia vitu
vya kushikika tu (materials). Na wao wapenzi wapenda pesa pia wana
maswali yao wanayopenda kuyauliza mara kwa mara ili tu kuweza kuujua
umuhimu au nafasi yako kiuchumi ya kuweza kumsaidia, utawasikia
wakiuliza maswali kama vile; Je wewe unafanya nini kimaisha? Unafanya
kazi wapi? Unaishi wapi? Kama unafanya biashara wata tamani kujua mtaji
wako ni kiasi gani au kama nikazi basi watadadisi wajue unalipwa kiasi
gani, watauliza kama unagari? Na nigarigani? Wanapenda kuangalia hata
uthamani wa simu ya mkononi unayoitumia, na maeneo gani unapenda
kustarehe. Vitu vyote hivi vitamwezesha kuujua uchumi wako na kufahamu
kama akitua kwako atapeta au atapatwa? Baadhi
ya matatizo ambayo mpenzi mpenda pesa zako atayaopoa ni kama vile shida
ya kodi ya nyumba, gari yake imeharibika umsaidie kuitengeneza na kasha
atakulipa, mdogo wake au ndugu yake anatakiwa ada ya shule na kwa sasa
yeye hana kitu, mara nyingine hata siyo ada ya ndugu yake yeye mwenyewe
anaweza kuomba ada kwako kama vile wewe ni mzazi wake. Moyoni mwake
anajua kabisa unampenda na huwezi kuona anafukuzwa kwenye nyumba sababu
hana kodi na hivyo utalazimika kumsaidia, hata kama ameahidi kukulipa
maranyingi utaambulia ahadi tu, na kama alijaribu kuanza kukulipa deni
Fulani basi kamwe hatomalizia pesa zote alizo ahidi. Angalia sana
usijeuzwe ATM, au saccos. Mpenzi
wa tabia hii kamwe hapendi uzungumzie matumizi yake makubwa, yeye
anataka kutumia tu hela yako, atanunua vitu na kutoa oda kubwakubwa ili
wewe ulipie, ukitaka kugombana nae muulize mbona matumizi yako makubwa?
Atakwambia kama penzi limeisha moyoni mwako si umwambie tu? Na wewe
unabaki huwezi kusema bali unaumia tu, hii mbaya sana!Mpenzi
mpenda pesa zako wakati wowote wanajihisi wanahaki ya kupewa, na
wanastahili vya thamani ingawa wao hawaonyeshi uwezo wa kuvitengeneza
kwa ajili yao wenyewe bali watawaegemea wengine ili wawawezeshe kuishi.
Kama unataka kujiepusha na mpenzi mpenda pesa zako basi usijionyeshe
kuwa unavijisenti unapokuwa naye kuanzia mwanzoni kabisa. Asikuone na
usafiri wa garama au mavazi ya anasa, jiepushe na vyote vinavyoionyesha
thamani yako kwasababu hivyo ndivyo wanavyovitafuta. Nikuulize swali;
kwani hujawahi kuona kijana wa kiume kila mpenzi aliyenae ni mwenye
uwezo, anagari, labda ananyumba au anajenga au ametokea kwenye familia
bora? Je haujawahi kuona binti ambaye kila mpenzi wake lazima awe na
maisha fulani, gari zuri au afanye kazi nzuri? Yamkini unawajua hata
majina yao watu hawa, au hata ni wewe mwenyewe ninazungumza nawe. Fahamu
haujengi bali unabomoa, badilisha mtazamo.