simu
nyingi za juu ambazo zina specification za ukweli zinauzwa bei kubwa
approximation ni millioni moja kwenda juu. mfano wa simu hizo ni kama
nokia lumia 920, samsung galaxy s3, htc droid dna na iphone 5. lakini
ukiangalia kwa makini unakuta vitu vingi vinavyofanya hizo simu ziuzwe
bei kubwa havina maana kwa mazingira ya kiafrica.
mfano network ya 4g(lte), kustream hd(network yetu ipo slow), vitu kama
gps hatutumii na mambo ya location, wengi wetu hatujali toleo la
operating system kama ni android hata ikiwa 2.3 inatosha.
kutokana na mambo hayo nikaona niandae hii makala ya kuonyesha aina za
simu ambazo kimuonekano ni kama simu za bei ya juu lakini zimenyimwa
vitu flani ambavyo si muhimu kwa muafrica kuvikosa na hivyo kufanya bei
ishuke. kwa kubase kwa ukubwa wa screen (zaidi ya 4.2 inch) na udogo wa
bei (china ya laki 5)
kambi ya htc
hapa kuna simu moja tu
htc inspire 4g
kwanini ununue?
kwa sababu ina screen ukubwa 4.3 yenye resolution ya 480x800, ina
gorrila touch screen inayofanya kioo kiwe kigumu kuvunjika. ukubwa wa
screen umeizidi iphone 5 na imepitwa kidogo tu na samsung galaxy s3 pia
inauwezo wa kuchukua semi hd video 720p na camera ya 8mp.
general perfomance
inakubali android hadi 2.3 gingerbread ikiwa na processor ya 1ghz na ram
786 na internal memory ya 4gb ikisuport memory card ya 32 gb (memory
card ya 8gb inakuja na simu). kwa specification hizo zinaifanya hii simu
kuwa fair, itarun smooth. pia ina speed hadi 14.4 mbps kwenye internet
kwa standard ya 7.2 mbps kwa tanzania simu itakua very fast.
kambi ya samsung
tuwe wa kweli ni vigumu kupata samsung kwa bei rahisi nyingi zinauzwa
bei kubwa sana hapa nimepata simu moja tu ambayo haina 3g.
samsung galaxy s wifi
nisiizungumzie sana maana haina 3g wala haitasuport function zozote za
simu lakini hii inaweza kua mbadala wa ipod maana ina kioo kikubwa cha
inch 5, na storage ya 16gb au 8gb so ni nzuri kuangalizia movies, videos
, kuhifadhi picha, kuskilizia miziki na kuchezea games.
kambi ya kaka lenovo
lenovo a800
huyu jamaa lenovo anakuja juu sana mwaka jana ilikua ndo kampuni iliouza
sana computer na kwenye simu akampita nokia na samsung kwenye soko la
china. hapa anakuja na simu yake a800, ikiwa na screen ya 480x800 kwenye
kioo cha 4.5 inch na ram ya 512mb pamoja na processor 1.2 ghz dual core
na operating system ya ice cream sandwitch inaifanya hii simu kuonekana
bora zaidi.
bei pia sio mbaya sana kwa simu hii maana ni chini ya laki 4
kambi ya micromax
micromax a110
wengi labda mtakua wageni wa hii kampuni lakini ni kampuni ya kihindi
ambayo inatengeneza simu cheap sana za android na hii a110 ina screen
5inch ukubwa kama galaxy note ikiwa na resolution ya 480x800 na ram ya
512 mb. processor ni 1ghz dualcore na internal memory ni 4gb. hii nayo
bei ni chini ya laki 4.
kambi ya ACER
acer liquid gallant e350
hii ndo simu ya MWISHO ikiwa na screen ya 4.3 ina internal 4gb ram 1gb na proccessor 1ghz. resolution kidogo kubwa ina 540x960
kwa hisani ya my bast friend Cheaf kwawa jf member
Categories: