Ndugu mwana blog leo tumebahatika kuwaletea mahojiano na ndugu Geophrey Tenganamba ambaye ni
mkurugenzi
mwanzilishi wa Perfect Path Innovators tuunganewote kama utakuwana maswali usisite kuuliza au kumuulizandugu yetu hapa nayeye ataujibu
1-Tafadhali tupe japo
historia yako kwa ufupi?
Mimi ni Geophrey Tenganamba, mtoto wa tano katika familia ya
Marehemu Mzee Antony Tenganamba, ni mzaliwa wa mkoa wa rukwa lakini kwa sasa
makazi na biashara zangu zipo hapa Dar es salaam na morogoro. Nina Shahada ya
Uhasibu na masoko niliyoipata kutoka
katika chuo kikuu Zanzibar,2009. Ni mshauri wa maisha au mwanamapinduzi
wa maisha, biashara,mahusiano na uwekezaji. Ni mhasibu wa tume ya vyuo vikuu,
mkurugenzi mwanzilishi wa Perfect Path Innovators inayotoa huduma na utalaamu
wa biashara na masoko,computers na
mengineyo. Ni mhamasishaji mwenye kipawa kikubwa na nimefanikiwa kufanya semina
na Erick Shigongo, Chriss Mauki,Felix Majangilla na wengine wengi. Ninapenda maisha
ninapenda kuishi tofauti na kuonyesha tofauti.Ni mtunzi wa vitabu vikubwa hapa
nchini na watu wanavinunua sana; kama “Kichwa Chako Ni Dhahabu ya utajiri”, the
richest Goldmine in You na Nguvu ya kujitajirisha ndani yako. Vipo sokoni.
2-ni jambo gani ktk maisha unapenda kulifanya au unajutia kulifanya?
Napenda kuishi,
sana kuishi kwa malengo na kusababisha kitu kwa binadamu wanaonizunguka.
Nimewahi kufanya makosa lakini kamwe sipendi kujuta, hakuna jambo ninalolijutia
maishani.
3-hivi mafanikio ya kweli yanaweza kupatikana nje ya MUNGU?
3-hivi mafanikio ya kweli yanaweza kupatikana nje ya MUNGU?
Binadamu wote wapo ndani ya Mungu, ndani ya duara la Mungu,
na hakuna mtoto wa shetani hapa duniani. Kila binadamu anaweza kufanikiwa, ila
kufanikiwa kwa njia ipi na kwa matakwa ya nani ni muhimu. Na mafanikio ni
kulingana najinsi mtu mhusika anavyoyachukulia, yeyote Yule ambaye anasema
amefanikiwa lakini hajui amefanikiwa kwa matakwa ya nani hajafanikiwa bado,
mafanikio ni pamoja na furaha ya moyo, tumaini la kufika huko tuendako na fedha
za kukutosha na kuwasaidia wengine. Kila mmoja anaweza kufanikiwa lakini lazima
achukue hatua kwanza.
4-kwa nini wasomi wengi wa hapa nchini wanapenda kuajiriwa kuliko kujiajiri?
4-kwa nini wasomi wengi wa hapa nchini wanapenda kuajiriwa kuliko kujiajiri?
Wasomi wengi
wanapenda kuajiriwa kwasababu ya mazoea waliyoyakuta, mara nyingi sana msomi
akiamua kujiajiri huonekana kama anapotea. Ni aina ya uoga wa wasomi wengi, na
uoga ndiyo mchawi mkuu wa mafanikio ya binadamu yeyote. Kuajiriwa ni raisi
lakini matunda yake ni madogo au twaweza kuita ni makaburi ya vipawa na uwezo
wa binadamu. Binadamu anayefikiri na kukumbana na mambo katika kujiajiri
hufufua uwezo wa ndani yake na kuwa mkubwa hata kiakili. Hivyo ni uoga tu wa
kuona makubwa. Nchi hii ina fursa nyingi sana kama wasomi wakiamua kujiajiri.
5-nini ushauri wako kwa wasomi wa hapa nchini kwetu?
5-nini ushauri wako kwa wasomi wa hapa nchini kwetu?
Tanzania bado inahitaji binadamu wanaodiriki, wanaoamua
maisha yao kwa mfumo wanaoamini wao hasa kwa kujiajiri. Ni muhimu sana kuwa na
tabia ya kutaka makubwa ili upate makubwa; kwa mfano
“Mpaka lini utaendelea kuwa mtumishi wa wahindi kama punda
wakati uwezo wa kuyatengeneza makubwa kama wao unao? Kwanza nchi ni ya kwako ni
vema utumie fursa hiyo. Kuna siku tulikutana na MODESTA MAHIGA, aliniambia kuwa
hakuna nchi raisi kujiajiri na kupata makubwa kama Tanzania, ukishaamua kuwa na
ndoto yako na kung’ang’ania kuifikia.
6-nini siri ya mafanikio yako?
6-nini siri ya mafanikio yako?
Ni kuamua tu, yaani
unaamua unachotaka na unahakikisha kinapatikana basi. Naomba wasome link hii
katika blog yang kujua nini maana ya kuamua
http://treasurehousewithinyou.blogspot.com/2011/11/amua.html
7-Unajisikiaje pale unapofanya kitu na kukifanikisha?,na kama
haujakifanikisha unajisikiaje?
Najisikia kufurahi,
nauona uwezekano wa kuyafanya mengine zaidi. Kuhusu kutofanikisha, yakitokea
hayo najiona kuwa nahitaji kuongeza mwendo zaidi.
8-Upi ushauri wako kwa mtu ambaye anafanya kitu na kushindwa kukifanikisha?
8-Upi ushauri wako kwa mtu ambaye anafanya kitu na kushindwa kukifanikisha?
Hakuna binadamu aliyewahi kukuta vitu mteremko, lazima
alijaribu akashindwa, akajaribu kwa njia nyingine akashindwa tena, lakini
hakukata tama na mwisho wa siku akashinda. Huwezi kusema umeshinda wakati
hakuna jasho ulilotoa. Maisha siyo rahisi, lakini yanawezekana kwa Yule
asiyekubali matokeo na kuanza tena.
9-nasikia wewe ni mwandishi wa vitabu? kama ni kweli umeshaandika
kitbu kipi na kipi?
10- pia wewe ni Director and founder of Perfect Path Innovators,hii
inausika na nini hasa?
9-nasikia wewe ni mwandishi wa vitabu? kama ni kweli umeshaandika
kitbu kipi na kipi?
10- pia wewe ni Director and founder of Perfect Path Innovators,hii
inausika na nini hasa?
Inatoa ushauri wa biashara, masoko, uwekezaji na mengine
mengi kama nilivyosema mwanzo kaka Godlisten
11- kama mtu akihiitaji kitabu chako anaweza kufuata utaratibu upi? ua
vinauzwa wapi?
11- kama mtu akihiitaji kitabu chako anaweza kufuata utaratibu upi? ua
vinauzwa wapi?
Vitabu nilivyotunga
ni kama kichwa chako ni dhahabu ya utajiri, nguvu ya kujitajirisha ndani yako,
the richest goldmine in you. Kwasasa vimeisha bookshop lakini tumeshaanza
kuvisambaza tena. Lakini kwa anayehitaji, anaweza kupiga simu +255714477218,
email:gtlivemore@gmail.com, ataletewa mahali popote alipo. Na kwa taarifa zaidi
wapite katika blog hii: http://treasurehousewithinyou.blogspot.com/search/label/SWAHILI%20INSPIRATIONS
Asante
asante ndugu Tenganamba kwa ushirikiano wako
Categories:
nice one i like this interview..
kazi nzuri nimeipenda hii!!!
Asanteni sana kwa kuonyesha ushirikiano blogger wa Wamtaani
asante dada Yasinta.
karibu tena hapa na nafikiri muda si mrefu utakuwa mwoja wao tunakusomakama hivi