1. Jiwekee malengo ya kifedha
Weka
maamuzi binafsi ya nini unachokihitaji na wapi unakotaka uwe kimaisha
hapo mbeleni. Yaweke malengo yalio ya kifedha katika makundi yafuatayo
- Malengo ya muda mfupi
- Malengo ya muda wakati
- Malengo ya muda mrefu
Malengo
haya yanaweza pia kugawanywa kufuatana na mahitaji uliyonayo. Vile
vyenye uhitaji mkubwa vikapewa umuhimu katika malengo n.k. Tafiti za
maeneo mbali mbali zimejaribu kuweka mifano ya malengo haya kama
ifuatavyo.
Mipango ya muda mfupi (short term goals)
- Kununua gari jipya (ingawa hii hutegemea na uwezo binafsi)
- Kuandaa harusi
- Kuendelea na shule ya juu (Graduate school)
Malengo ya muda wakati (Mid term goals)
- kupata watoto
- kujenga nyumba
- kuanzisha biashara
Malengo ya muda mrefu (long term goal)
- Kuweka fedha kwa ajili ya kustaafu (NSSF, PPF, Saving Account)
- Kujenga nyumba kwa matumizi ya likizo (vacation home)
- Kufungua akaunti ya watoto wakiwa wadogo
2. Tengeneza fungu la fedha la dharura
Wengi
wetu hatuna tabia za kujiandaa kwa majanga na dhama mbali mbali na
hivyo mambo haya yanapotokea tunakuwa katika hali mbaya zaidi. Hii ndio
maana wengi wetu wanapojikuta wako katika misiba, au majanga mbali
mbali, hukimbilia kukopa au kuchukua advance za mishahara nahii huwaacha
wengi katika madeni sugu.
Fikiri
ni kiasi gani cha fedha kinahitajika kwa majanga au dharura ambazo
zaweza kutokea katika mzunguko wa maisha ya kila siku. Inashauriwa kuwa,
ujaribu kuweka fedha inayolingana na matumizi yako ya mwezi kwa miezi 3
– 6 kama fungu la dharura. Hii ni fedha ambayo itakuwa tayari kutumika
mara tu upatapo dharura yeyote kama vile, Ugonjwa wa mwanafamilia, ajali
kupoteza kazi, msiba wa ghafla n.k. (najua wengine wenye imani zao wana
mitazamo tofauti na hili lakini piga hesabu jinsi unavyosumbuka na hata
kusumbua wengine pasipo sababu muhimu pale dhahama inapokukumba na
haujajiandaa hata kidogo.
3. Anza kuwekeza
Hatua
ya pili ya kuandaa fungu la dharura na majanga ni lazima iwepo tayari
kabla hata haujaanza kuwaza kuwekeza. Kuwekeza kunatupa kipato cha
nyongeza ili kutia nguvu kile kidogo kinachopatikana toka kwenye
mshahara au fedha ulizojiwekea benki hii inakusaidia kuanza mchakato wa
kuwa tajiri.
4. Anza kuwekeza kwa maandalizi ya kustaafu
Hii
ni zaidi kwa wale wanaofanya kazi katika ajira mbali mbali za kuajiriwa
pamoja na waliojiajiri. Takwimu zinaonyesha kuwa, mtu wa maisha ya
kawaida anahitaji asilimia 70% za kipato chake cha kabla ya kustaafu ili
kumsaidia kuendelea maisha katika hali ile ile aliyokuwanayo, mara tu
atakapo acha kufanya kazi. Mfano; Mtu anayepata sh. 500,000 kwa mwezi
atahiraji shilingi 350,000 kwa mwezi mara atakapoacha kufanyakazi ili tu
kuweza kuishi maisha ya aina angalau sawa na aliyokuwa akiishi kabla ya
kuacha kazi.
Fedha
za malipo ya uzeeni pensheni (NSSF, PPF) hazitoshi kukidhi mahitaji
yako hata kidogo. Na inabidi usisahau kuwa takwimu zinaonyesha kuwa mtu
wa kawaida anategemewa kutumia 1/3 ya maisha yake yote katika muda wa kustaafu kazi (muda ambao hata mwili wako hauwezi kuzalisha kama awali)
5.
Piga hesabu ya uwezo wako wa kuwa tayari kupoteza; je ni kwa kiasi gani
uko tayari kupoteza. (How much are you ready to take risk?)
Tafiti
zaonyesha kuwa watu wenye umri mdogo wana uwezo wa juu wa kukubali au
kuwa tayari kupoteza (taking risks) kuliko watu wazima. Pia takwimu
zinaonyesha kuwa wengi waliofanikiwa duniani walikuwa tayari kupoteza.
Huwezi kujiita mfanyabiashara kama hauna ujasiri wa kuwa tayari
kuziwekeza fedha zako katika mtaji ambao hauna uhakika wa kurudisha
faida. Inahitji kiwango cha juu sana cha kukubali kupoteza na kuwa
tayari kupata hasara. Kwa ajili hii ili uweze kupata upenyo mapema
unashauriwa kuanza kuwekeza ukiwa kijana wakati ambapo uwezo wako wa
kukubali kupoteza uko juu, kinyume na kusubiri ukiwa mtu mzima sana
wakati ambao utakuwa unahofia kila kitu unachokiona au kukiwazia.
Kwa hiyo: Fahamu
uwezo wako wa kuwa tayari au kukubali kupoteza. Fahamu uwezo wako wa
kuweza kuvumilia pale hasara yakupoteza inapotokea. Umri wa ujana unampa
mtu uwezo mkubwa kwa kuwa tayari kujaribu vitu vipya mara kwa mara, na
kuweza kujirekebisha kwa urahisi pale makosa yanapotokea kuliko umri wa
utu uzima sana. Wakati ambapo majukumu huzidi idadi ya nywele za
kichwani na kiwango cha msongo wa mawazo huwa juu sana.
Na: Chris Mauki
University of Pretoria
South Africa
chriss@udsm.ac.tz
Categories:
I was following you session with Joyce Kiria at Wanawake live show,, I real like it, thanx much bro. Keep the fire burning, soo many relations break because they could'nt sort what are their differences and behavious that can be controlled and changed.
stay blessed
Nei...
ASANTE.
Natamani sana kufanikiwa, nawaza sana.