WAKUU LEO NIMEWEZA KUTEMBELEA MAONYESHO YA KIMATAIFA YA DAR NA NILI CHOMOKA KUTOKA ARUSHA ILI NIJE DAR KUHUDHURIA ANGALA SIKU MOJA, Kwa kweli Manonyesho ni Mazuri sana, na yanavutia sana na kama yakitiliwa manani yana weza sana kuwasaidia Watanzania kupiga Hatua za Kibiashara, SASA NIANZE NA MAZURI NILIYO YAONA KULE VIWANJA VYA SABASABA 1. Idadi kubwa sana ya Watu wanaotembelea yale Mainyesho 2. Makampuni mengi 3. Makampuni ya Kitanzania kuonyeshaubunifu wa hali ya juu 4. Ulinzi wa kutosha MAPUNGUFU NILIYO YAONA MIMI 1. Maonyesho kugeuzwa kuwa SOKO AU GURIO, kinacho endelea pale ni mauzo kuliko manunuzi 2. Makampuni ya Tanzania kuwa machache sana na mengi kurudia rudia bidhaa za miaka miatu iliyo pita- Ukiangalia kwenye Mabadna karibia yote ya Bidhaa za Tanzania utagundua ni zile zile za miaka minne mitatu iliyo pita, it means hatuna Ubunifu tena, ndo tumefikia mwisho wa kubuni 3. Watanzania wengi wanao hudhuria maonyesho kujikita katika kununua kuliko kupata elimu- Kwa kweli idadi ya Wahudhuriaji wanaenda kununua na si kupata elimu, wengi wako bize kununua Vyombo vya Ndani na kazaila 4. Makampuni ya Kitanzania na watanzania wanaoshiriki kuonyesha Bidhaa za kitanzania kujikita katika kuuza sana na si kutafuta wabia wakufanya nao Biashara - WATANZANIA WAKO BIZE KWENYE KUUZA NA SI KUONGEA NA WATU NA KUWAACHIA CONTACT ILI WAFANYE NAO BIASHARA 5. Maonyesho kutawaliwa na Bidhaa za kichina zaidi HAYA MAONYESHO UNAWEZA ZANIA UKO CHINA MAKE BIDHAA ZA CHINA NI NYINGI SANA KULIKO ZA TANZANIA NA HATA NCHI ZINGINE 6. Wachina Kuwa makini sana na kilicho waleta Tanzania WACHINA WAO WAMEKUKA KUTAFUTA MASOKO NA SI KUUZA NA UKIINGIA KWENYE YALE MABADA YAO HAKUNA KINACHO UZWA ILA WAKO BIZE NA MADAFUTARI YAO KUCHUKUA CONTACT ZA WATU ILI WAFANYE NAO BIASHARA 7. SWALA LA CUSTOMER CARE- wachina na wahindi wako juu sana katika kuongea na Wahudhuriaji na kujaribu kuwafafanulia bidhaa na huduma wanao toa 8 Watanzania CUSTOMER CARE YETU NI KAMA KAWAIDA TUKO BIZE KUSOMA MAGAZETI NA KUCHATI NA SIMU- Inasikitisha sana Watanzania badala ya kuja kupambana kwenye maonyesho tumekuja kuuza sura na kusoma magazeti, MIMI NILIINGIA KWENYE BAADHI YA MABANDA LIKIWEMO LA SIDO, sikupata mtu wa kunipa maelezo ya nilicho kuwa na taka kisa eti anaongea na simu huko nje, HEBU FIKILIENI WAKUU Kwenye Mabanda ya SERIKALI NDO USISEME, wanakutazama kama umefuata misaada pale wako bize wanapiga story za siasa kwenye maonyesho badala ya kutoa elimu, 9. Watanzania wengi kujikita kutembelea MABANDA YA BIDHAA ZA KICHINA NA ZA ANASA KAMA MABANDA YA KUUZA FANICHA ZA KICHINA, VYOMBO, MIKUFU NA KAZALIKA, na kuacha MABANDA YENYE KUTOA ELIMU NZURI KAMA YA SIDO, MAGEREZA, VETA, JKT NA KAZALIKA 10. Bidhaa nyingi za KITANZANIA KUJIRUDIA KWENYE MABANDA MBALI MBALI- Ukichunguza kwa umakini unaweza ingia banda la SIDO ukakuta Bidhaa ambayo utaenda kuikuta hiyo hiyo Banda la WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA NA MABANDA YA ANA MKAPA NA KAZALIKA na utaikuta na hiyo hiyo nembo na mwenye kuuza atakomaa yeye ndo anatengeneza, HAPA NI KWAMBA WAONYESHAJI WENGI WANANUNUA BIADHAA NA KWENDA KUUZA PALE UWANJANI NA SI KUONYESHA UBUNIFU WAO, Maoni Yangu ni haya 1. Serikari na waandaaji wapige Marufuku kuuza bidhaa mule ndani na watu wajikite katika kutangaza na kutafuta masoko, 2. Waandaaji wahakikishe wanaoshirika wana Uelewa wa kutosha wa bidhaa wanayo onyesha na si kwenda kuuza badala ya kuonyesha 3. Watanzania wajitahidi kuja na vitu vipya kila maonyesho na si kurudia vitu ambavyo viko mitaani mida yote, KWA MABANDA YA WATANZANIA UTAGUNDUA VITU KAMA UNGA WA LISHE, SIAGI, SABUNI, VIKOI, SHANGA, NA KAZALIKA VIKO MITAANI KWA WINGI SASA KULE WANAENDA KUONYESHA KITU GANI WAKATI BIDHAA TUNAZITUMIA MITAANI? MWISHO KABISA TUJITAHIDI SANA KUNUNUA BIDHAA ZA KITANZANIA WAKUU MAKE ZINA VIWANGO HATA KUZIDI ZA WAZUNGU TATIZO NI UBUNIFU NA MITAJI NDO TATIZO BIDHAA KAMA ZA 1. VETA- Wana bidhaa za ubora wa hali ya juu kabisa 2. JKT 3. MAGEREZA 4. SIDO KAMA SISI TUSIPO NUNUA WATAPATA WAPI PESA ZA KUFANYIA INOVATON ZAIDI? source:KOMANDOO jf member

Categories:

Leave a Reply