KUKATA tamaa na kukosa tumaini kunaweza kukuongoza katika kufikiria hali ya kutaka kujinyonga. Lakini kumbuka kuwa una njia mbadala/suluhu nyingine zinazoweza kukusaidia kuepuka mara moja mgogoro huo na zikakusaidia kuibua mpango wa usalama wa muda mrefu.
Kuna wakati inapofikia hatua na kuona kuwa hakuna umuhimu wa kuishi, au matatizo yako yanaonekana kuwa mengi, kutokana na hali hiyo, hivyo unafikia hatua na kuona njia pekee ni kujinyonga.
Unaweza usiamini, lakini unaweza kuwa na njia nyingine itakayokufanya uendelee kuishi na kujisikia vizuri juu ya maisha yako, endapo utakuwa umefikia hatua ya kutaka kujinyonga.
Mara nyingine unaweza kufikiri kuwa umeshajaribu njia zote za kuondokana na hali hiyo ya kutaka kujinyonga, bila mafanikio, na kuona kuwa familia na rafiki zako wanakutenga.
Ni sawa kujisikia vibaya, lakini jaribu kutenganisha hisia zako na vitendo vyako kwa wakati huo. Tambua kuwa hali hiyo ya huzuni uliyonayo au mawazo uliyonayo au hali ya kukata tamaa ya muda mrefu uliyo nayo inaweza ikakugeuza vibaya mwelekeo wako kuondoa uwezo wako wa kufanya maamuzi.
Hisia za kujinyonga ni matokeo ya ugonjwa usiotibika. Kwa hiyo jaribu kuonyesha kuwa kuna uwezekano mwingine, hata kama hujauona kwa sasa.
Inaweza ikawa si rahisi kuondoka katika hali hiyo iliyokupata hata ikakusababisha usijisikie vizuri usiku kucha. Kutokana na hisia hizo ulizonazo za kukata tamaa, unaweza ukapata njia ya kutafuta ufumbuzi mpya kama matibabu na sababu za wewe kuishi.
Jitahidi kila siku uwe na mbinu za kuzuia hali hiyo kwa kuzungumza na daktari, familia au rafiki zako waweze kukusaidia kuondokana na hali hiyo.
Mbinu hizo zitakuwezesha kufanya vitu ambavyo hujisikii kuvifanya, kama kuzungumza na marafiki wakati umekuwa chumbani kwako siku nzima huku umeteremsha mapazia. Au unaweza kwenda hospitali kwa daktari wa akili kwa ajili ya kukufanyia tathmini. Lakini zingatia mbinu hizo, pale unapokuwa umevunjika moyo na kukosa matumaini.
Moja ya mbinu hizo ni kutunza orodha ya majina na namba zinazoweza kupatikana kwa urahisi, zikiwamo za madaktari, familia na ndugu zako ili endapo utakuwa na hali hiyo uweze kuwasiliana nao.
Kama malengo yako ya kujinyonga yanaendana na kunywa vidonge, hii inamaanisha kuwa badala ya kunywa vidonge viwili ulivyoelekezwa wewe unakunywa zaidi ya maelekezo ya daktari. Ni vizuri kutoa maelekezo yako ya dawa ulizonazo kwa yeyote anayeweza kutunza dawa zako na anayeweza kukupa dawa hizo kwa wakati, kuondokana na hali hiyo ya kujizidishia ambayo itakusababisha madhara.
Pia waweza kuondoa nyumbani kwako vitu vyote vya hatari kama visu, risasi, wembe au silaha nyingine zozote mtu anazoweza kuzitumia katika uharibifu wa maisha yako.
Hivyo ni vizuri ukawa na ratiba yako ya kila siku itakayokufanya uwe na shughuli na kukusahaulisha yaliyopita kama kutembea mwendo mfupi, kusikiliza muziki, kuangalia sinema inayovutia, na kutembelea maeneo ya makumbusho.
Baada ya kufanya yote hayo kama hutapata walau furaha kidogo, jaribu kitu kingine tofauti kitakachoondoa maumivu yanayokukabili. Jaribu kuwa pamoja na watu wengine, hata kama hujisikii kuwa nao, ili kuondoa hali ya kujitenga.
Epuka mihadarati na pombe. Zaidi ya kupata hisia za ganzi mwilini, pombe na mihadarati inakuongezea maumivu, unajiingiza zaidi kwenye kujidhuru mwenyewe au kuwa na wakati mwingine kuchanganyikiwa.
Andika kuhusu mawazo na hisia zako. Kumbuka pia kuandika vitu katika maisha yako ambavyo unavithamini na kuvikubali. Haijalishi ni kwa udogo gani unavyoviona.
Unapokuwa katika hali hiyo ya mawazo ya kujinyonga, kabla hujaamua kufanya hivyo, zungumza na mtu yeyote kama vile, kupiga simu kwa rafiki yako au huduma ya simu za dharura.
Kama hutaki kufanya hivyo kutokana na sababu yoyote ile, njia nyingine ni kuwasiliana na daktari wako, kiongozi wa dini au yeyote uliyenaye katika imani yako.
Zungumza na yeyote kuhusu hisia zako, kwani anaweza kukusaidia kukupa nafuu katika mzigo ulionao wa kuvunjika moyo na upweke, hata kama ni msaada wa muda. Itakusaidia kuhamisha mtazamo na kuona kuwa upo uwezekano mwingine zaidi ya kujinyonga.
Pia, zingatia kuweka ratiba maalumu ya shughuli ambayo utajaribu kuifuata wakati unajisikia vibaya. Ufunguo wa tatizo hilo ni kujiingiza kwenye shughuli mbalimbali kama kikwazo cha kuruhusu mawazo mabaya. Pia, uhakikishe kuwa shughuli hizo zinakupatia furaha na kukupa faraja, siyo kukuongezea msongo.
Jaribu kufanya haya ili uweze kujihisi kuwa unapenda kuendelea kuishi. Fanya zaoezi la kupumua pumzi kutoka ndani, piga muziki wa ala, oga kwa maji ya moto, kula chakula kizuri ukipendacho, andika jarida, fanya matembezi, wasiliana na familia, marafiki au wasiri wako unaowaamini.

Categories:

Leave a Reply