WAKATI mwingine, hasira na kuchanganyikiwa kwetu kunasababishwa na matatizo yasiyozuilika katika maisha yetu ya kila siku.
Si kila hasira haina mpangilio, na mara nyingi inatokana na mambo ya kiafya, ni hali ya asili inayojitokeza katika mambo tunayokutana nayo.
Njia sahihi ya kukabiliana na tatizo linalokukabili, ambalo linakusababishia hasira, si tu kulenga katika kutafuta muafaka, lakini zaidi ni jinsi gani ya kulichukua na kukabiliana nalo.
Kutatua matatizo yanayokusababishia hasira kutaleta matokeo mazuri, lakini pia si kujiadhibu mwenyewe kama jibu halitakuja kama ulivyotarajia.
Watu wenye hasira mara nyingi hurukia jambo na kulifanyia maamuzi, lakini baadhi ya maamuzi hayo yanaweza yasiwe sahihi.
Kitu cha kwanza cha kufanya kama upo kwenye majadiliano makali ni kupunguza hasira na kufikiri juu ya majibu yako unayoyatoa.
Katika majadiliano hayo, kamwe usiseme kitu cha kwanza kinachokujia kichwani pako, bali tuliza hasira na fikiri kwa uangalifu juu ya kile unachotaka kukisema. Wakati huo huo, sikiliza kwa makini mtu mwingine anachokisema na jipatie muda kabla ya kujibu.
Pia sikiliza kwa makini, jambo lile linalokusababishia hasira. Kwa mfano, wakati mwingine unahitaji uhuru wako binafsi, wakati huo mke au mume wako anahitaji mawasiliano ya karibu na wewe.
Kama ataanza kulalamika kuhusu tabia zako, usilipize kisasi kwa kumfananisha na mfano usio mzuri, kwani hali hiyo italeta uharibifu katika uhusiano wenu.
Ni jambo la kawaida kwa mtu yeyote kujilinda wakati anapokosolewa, lakini akumbuke kuwa makini, asiruhusu hali ya kupigana.
Badala yake asikilize kinachojili juu yake. Ujumbe wa mtu huyo unaweza ukaudharau na kutoupenda.
Utahitaji uvumilivu kwa upande wako, na inahitaji kuvuta pumzi, lakini usiruhusu hasira yako au ya mshirika wako aache majadiliano yawe katika udhibiti. Kutulia kutaifanya hali kutokuwa ya uharibifu.
Wakati mwingine, ni vizuri kutumia ‘vichekesho’ kwani vinaweza kukusaidia kupunguza hasira katika njia mbalimbali. Kwa jambo moja la uhakika, ni kwamba vinaweza kukusaidia kuwa na mawazo yaliyo sawa.
Hivyo, wakati unapokuwa na hasira halafu unamwita mtu fulani jina au kumfananisha na kitu fulani, acha na ufikirie neno hilo linafananaje.
Fanya hivi pale jina linapokujia kwenye kichwa chako kuhusu mtu mwingine. kama unaweza, fikiria picha ya kitu halisi kinavyokuwa.
Hali hii itakuondolea hasira uliyokuwa nayo, na vichekesho mara zote vinakuondolea hali ile ya ghadhabu uliyonayo.
Ujumbe muhimu kwa watu wenye hasira kali, Dk. Deffenbacher anasema, watu wenye hasira wana tabia ya kujihisi kuwa wana haki, lakini mwisho wao hujikuta wakiwa wamejishushia heshima mbele ya jamii, lakini hawakutakiwa kutaabika kwa njia hiyo.
Labda watu wengine wangeweza kufanya hivyo lakini si wao.
Wakati unahisi kuwa unataka kuwa na hasira, mtaalamu huyo anashauri, jifikirie mwenyewe kama ungekuwa ni Mungu au kiongozi mwenye mamlaka ya juu, ambaye unamiliki mitaa, maduka na maeneo ya ofisi, mwenye maendeleo ya haraka na kuwa na taratibu zako katika hali zote wakati wengine wanatofautiana nawe.
Jambo unaloweza kulijua zaidi katika mawazo yako, unajiona kuwa wewe si mtu wa maana, unaanza kuona vitu ulivyonavyo havina umuhimu hivyo unakuwa na hasira kutokana na ukweli huo.
Kuna tahadhari mbili za kutumia vichekesho. Kwanza, usijaribu kuondoa aibu yako kwa kucheka, badala yake tumia kichekesho ili kujisaidia kukabiliana na hali hiyo. Pili, usifanye jambo lisilopendeza, kichekesho cha kejeli, hiyo ni aina nyingine ya mwonekano wa hasira isiyo na afya.
Hasira ni hisia ya kuiangalia kwa umakini, lakini mara nyingine inakwenda na wazo kuwa kama utaichunguza, itakuwezesha ucheke.
Wakati mwingine hasira Inabadilisha mazingira yako. Kwa mfano mazingira yetu yanatufanya kuwe na misuguano pamoja na ghadhabu. Matatizo na majukumu yanaweza kukuongezea uzito na kukufanya upatwe na hasira.
Ipe nafsi yako mapumziko. Hakikisha una muda wako binafsi na ratiba inayokuongoza kwa siku nzima. Mfano moja ni kwa mama anayefanya kazi, ambaye amekuwa na sheria yake kwamba, wakati anarudi nyumbani kutoka kazini, kwa dakika 15 za kwanza hakuna yeyote atakayezungumza naye, baada ya muda huo mfupi wa mapumziko anajisikia vizuri na kuanza kuwaandalia watoto wake mahitaji yao kwa furaha.
Njia nyingine za kukupa ahueni katika maisha yako, ni kuwapo matukio tofauti tofauti ambayo yatakuondolea tatizo la hasira ulilonalo.
Muda - Kama wewe na mke au mume wako mmekuwa na tabia ya kutofautiana wakati mnajadili mambo mbalimbali muda wa usiku, Inawezekana mnakuwa mmechoka, au mna mawazo, au labda ni tabia yenu halisi, jaribu kubadilisha muda wakati mnaongea mambo muhimu, badala ya usiku iwe asubuhi au mchana.
Epuka - kama watoto wako wanaonekana wana fujo kwenye chumba chao, hali ambayo itakufanya ukasirike, inabidi ulifanyie kazi suala hilo kwa kukaa kimya na kufunga mlango wa chumbani kwako.
Tafuta njia muafaka - kama kila siku asubuhi unakutana na msongamano wa foleni, hali inayokusababishia hasira, ipe nafsi yako kazi ya kusoma ramani ya kujua barabara nyingine zisizokuwa na foleni. Au tafuta njia nyingine muafaka.
Kuna njia mbalimbali za kukuonyesha kuwa una hasira. Mwili wako utakujulisha kuwa una hasira, kwa kuhema kwa nguvu, kubadilika uso wako, kukaza kwa misuli yako pamoja na kuonekana unaongea kama unanguruma, hata kwa mtu unayempenda.
Watu wengine wanazika hasira zao ndani. Kama unafanya hivi, utapata maumivu ya kichwa au tumbo. Na mara nyingine unaweza kuanza kulia peke yako.
Si vizuri kuficha hasira yako, inakubidi utafute njia ya kuitoa pasipo kujiumiza mwenyewe au kuwaumiza wengine.
Kuna njia za kufanya endapo utajikuta kuwa umepatwa na hasira. Njia hizo ni kuongea na rafiki yako unayemwamini, kufanya mazoezi, kucheza michezo mbalimbali, kuimba, kupalilia bustani yako pamoja na kufikiria mawazo mazuri.
Kwa mtu yeyote mwenye afya, haiwezekani asipatwe na hasira. Badala yake ukumbuke kuwa, unapatwa na hali gani unapokuwa na hasira.
Je, inafanya mazingira yako kuwa mazuri au mabaya? Usiruhusu hasira iwe bosi wako. Fanyia kazi jambo hilo.

Categories:

Leave a Reply