Leo tutakwenda kuangalia jinsi unavyoweza kuonyesha zawadi ya upendo kwa watu, hata kama huna fedha.
Kila mtu anapenda kupendwa, yakupasa kuwa na rafiki wa karibu atakayekushirikisha katika mambo mbalimbali unayokabiliana nayo.
Hivyo ni vema kuwa na rafiki mzuri na kuonyesha upendo wako kwake, kwa sababu wakati mwingine unajikuta hata familia yako inakuwa mbali nawe, hivyo kipindi hicho unakuwa unahitaji mtu wa kuongea naye.
Pia ni muhimu kuwa rafiki mzuri kwa sababu unajifunza ni jinsi gani ya kukutana na watu wapya na unajifunza kutokana na makosa yako.
Tafuta watu ambao unapenda wawe rafiki zako, kwa kujitambulisha, kumwacha mtu mwingine kukueleza juu ya mambo anayoyapendelea.
Mwonyeshe mtu huyo kuwa unamwamini, mwache ajue kuwa ni sawa kupendana, mwache ajue kuwa uko pale kwa ajili yake na atakuwa rafiki yako wa kudumu.
Mara zote mfanye atabasamu hata kama ana huzuni. Pia mwache ajue kuwa upo tayari kusikiliza chochote atakachosema.
Je? Unawezaje kuonyesha upendo bila kutumia fedha? Wakati mwingine tunajitahidi kwa bidii kutafuta zawadi ambayo ni sahihi tunayofikiria kuwa ina maana kwa yule unayempelekea.
Au, tunaishikilia zawadi hiyo, tukifikiria kama kuna sababu maalumu ya kutoa zawadi hiyo. Ninakutia moyo kutoa zawadi yako kwa uhuru na iwe ni mara kwa mara, kumbuka kuwa utoaji ni shughuli ambayo inamnufaisha mtu kila mara anapofanya hivyo.
Tuangalie zawadi 10 ambazo zinafaa kwa siku ya kawaida na maalumu. Pia, ni zawadi ambazo mtu yeyote anaweza kutoa kwa sababu halazimishwi ila ni kwa nia ya kuleta ushirikiano.
Zawadi ya kwanza ni muda. Kumbuka kuutoa muda wako na kushirikiana na wenzako ni moja ya zawadi kubwa unayoweza kuitoa.
Kama unatoa dakika 10 kwa kupiga hadithi na mtoto wako, kupata chakula cha mchana na rafiki yako au kutumia muda wa mchana kwa shughuli za nyumbani, shambani au nyinginezo, ukiwa na mume au mke wako, unakuwa unajitolea nafsi yako na kujenga uhusiano mzuri kwa muda huo.
Zawadi nyingine ni kukiri kwa uaminifu. Tumekuwa tukisikia watu wachache wakisema kuwa wamepokea shukrani nyingi au pongezi nyingi.
Wote tunajisikia vizuri wakati tunapata taarifa nzuri na shukrani kwa vile tulivyo au tunayoyafanya.
Anza kuzingatia kuimarika katika hilo na kutoa sifa nzuri kwa wengine na kujenga tabia ya kukiri jambo zuri linalofanywa na wengine kwa kile unachokiona.
Nyingine ni Msamaha. Hii ni zawadi nzuri mno yenye nguvu. Wakati tunasamehe wengine, tunaacha kuwaadhibu. Tunawaruhusu ili wajisikie hatia au kuona aibu ili waweze kugundua makosa yao.
Msamaha pia ni zawadi ya kutuweka huru kutoka kwenye uzoefu ulioupata wakati ulipoumizwa moyo wako au maumivu katika matukio yaliyopita.
Vile vile upendo. Wakati unapotaka kuuonyesha upendo wako kwa wengine, usiwahukumu wengine, na uwaone kama ni watu wa muhimu kwako, watakatifu na wa thamani, hiyo ni zawadi kubwa.
Tunaposhiriki kwa uwazi upendo wetu na wengine inasaidia kuponya majeraha, kujenga uhusiano mzuri na kumsaidia mtu katika kupitia changamoto za maisha pia kuwa na maisha mapya ya uhakika.
Usiugawe usikivu wako. Ingawa tunatoa muda wetu kwa ajili ya wengine, akili zetu zinaweza kuwa popote kutokana na uzoefu.
Jiruhusu nafsi yako kuwa kwa mtu mwingine, kupanga naye shughuli nyingine, mawazo au ajenda mpaka utakapofikia malengo yako uliyokusudia.
Kama utafanya hivyo, watu watakuona unastahili kupata asilimia zote, kwa usikivu wako na kwa upande mwingine inawezekana ukawa hujafikia kiwango hicho ila kutokana na hali hiyo uliyojiwekea kwa watu.
Heshima. Mara kwa mara tunakuwa na shughuli nyingi au tunajishughulisha sana katika maisha yetu ambayo yamekuwa na matukio mfululizo ya kuvutia ambapo tunasahau kama kuna watu wengine wanaotuzunguka. Iache nafsi yako ipumue na kutoa heshima kwa watu ambao unakutana nao kila siku.
Yapo mambo madogo madogo ambayo yanaweza kufungua milango kwa watu wengine kuthamini mambo ambayo unawafanyia kama kumpa lifti kwenye gari yako, kumbebea gazeti lake mpaka mlangoni pake au kusimamisha gari lako mbele ya mtu unayemfahamu na kumpa lifti kipindi cha msongamano wa abiria kituoni.
Mambo yote hayo yataonyesha hali ya kujali kwa mtu ingawa wakati mwingine mtu hawezi kuelewa wema wako na kukushukuru.
Shtukiza. Zawadi za aina hii zinamfanya mtu kuwa mbunifu wa hali ya juu. Je, unataka kumpa dada yako kadi ambayo inasema unampenda? Unajisikiaje unapomtumia mumeo maua?
Je, ni kweli utamshtusha? Au labda umechagua kujitolea kumpa mfanyakazi mwenzako kigari cha kusukuma cha watoto ili aweze kufurahia jioni anapokuwa matembezi na rafiki zake?
Zawadi kama hizo zinakuwa tukio kubwa kwa yule unayempelekea katika siku yake ya kawaida kwa sababu hakutarajia kufanyiwa jambo kama hilo kwa siku hiyo.
Shukrani ni zawadi pekee kwa yule unayempa, kwani inasababisha mtu huyo kujua kuwa umekuwa makini kwa lile alilokufanyia. Kama ukiri wa dhati, na neno jingine ni kusema asante, linaonekana ni jambo ambalo si la kawaida.
Endapo utachagua kusema au kuandika shukrani zako, hii ni zawadi ambayo inakwenda ndani ya moyo wa mpewa shukrani.
Tabasamu katika dunia ya kisasa, mara nyingi tunaona tabasamu chache na nyuso zenye furaha ya kweli. Kinyume cha mwelekeo kwa kujivisha tabasamu kama sehemu yako ya kila siku.
Tabasamu linajulisha moyo mkunjufu, mapokezi na urafiki. Pia inafanya kuonekana kwa urahisi kwa wote wenye nyuso za tabasamu. Iache zawadi hii ya tabasamu itoe ujumbe. Mfano “Nina furaha uko hapa”.
Maombi ya kimya kimya. Wote tunakuwa na maombi ya ziada na ya baraka katika maisha yetu. Hata kama hufahamu, mtu mwingine anaweza kukubariki wakati unampa zawadi ya maombi yenye nguvu.
Kama unajua au la, mazingira ya mtu au dini yake, unaweza kuuliza kwa msaada au usikivu. Maombi rahisi unaweza kumwombea kwa kutumia “Mungu/Allah, ninakuomba umbariki mtu huyu na ukutane na mahitaji yake yoyote ambayo anayo katika maisha yake, asante”.
soursce:blog ya maisha yetu

Categories:

Leave a Reply