Kuna mambo muhimu na misingi bora ambayo kila kijana anapaswa kuyajua ili awe na mafanikio kwenye masomo na maisha yake kiujumla. Haya mambo ya mtu kujithamini (Self-esteem) na kujiamini (Self-confidence) yanaweza kumjenga mtu na usipoyatilia maanani yanaweza kumbomoa mtu. Leo tutaanza kwa ufupi kuelezea mada yetu umuhimu wa kuwa na mtazamo chanya wa kujijenga. Ukifuata Tips zote 5 tutakazo kudondolea, utakuwa kwenye ngazi ya kuelekea kwenye mafanikio ya hali ya juu. Umeshawahi kusikia mara nyingi watu wakisema “huyo hajithamini wala hajiamini”, lakini je, unajua maana ya maneno hayo?

Jinsi unavyo jithamini ni jinsi gani unavyo pima thamani ya utu wako. Kuna siku ambazo unaweza kuamka ari yako iko juu na unajisikia poa sana, unakuwa mwingi wa furaha, na unaamini kuwa ndoto zako zote zinaelekea unakotaka, maisha yako unayapa thamani na maana zaidi. Na mara NYINGI au chache kuna siku ambazo unaamka hujisikii vizuri kabisa, huna amani moyoni, huna furaha, tena una mashaka na kila ukifanyacho na kuona utu wako hauna thamani.

Kuna baadhi ya watu huwa na tabia ya kukosa ari (kujishusha) kila wakati, wao hujiona hawana thamani yeyote, hata ukikaa nao wanakutia unyonge, wana lalamika kila wakati - hii inasababishwa na kushushwa kwao thamani, eitha kwa fikra zao wenyewe au mtu au watu walio wazunguka. Kila mara watu hawa hujilinganisha na wengine (tena utakuta baadhi yao ni wacha Mungu sana), kufanya hivyo ni njia kubwa ya kushusha thamani yako. Unapo waangalia wengine na kufikiri kuwa “kwa nini mimi nisiwe kama fulani, mbona Mungu anampendelea hivyo”, pindi tu unapoanza kuwa na fikra kama hizi, basi jua kuwa umeshaukoleza moto wa kuushusha utu wako na utajisikia vibaya tu! Na pia kuna watu ambao ni eitha wenye kipato cha chini kabisa au walemavu, lakini ukikaa nao katika mazungumzo unakuwa na furaha sana kwa kuwa ni wachapa kazi, wacheshi, wanajiamini, wanauthamini utu wao, hawalalamiki na wanayakubali maisha waliyonayo na kukabiliana na kila hali, tena maisha yao yamejaa amani kuliko unavyotarajia. Yote ni juu ya kutumia mbinu hizi za kujithamini na kujiamini.

Tembelea ukurasa wetu wiki ijayo kuanzai Jumatatu tukijaaliwa tutakuletea mlolongo mzima wa mbinu ambazo zitakusaidia jinsi ya kujijengea tabia za kujiamini na kuachana na mawazo HASI ya kujishusha thamani. Tunakutakia siku njema!

Categories:

Leave a Reply